FT: Wiliete SC 0-3 Yanga SC

FT: Wiliete SC 0-3 Yanga SC

Dakika ya 88 nahodha wa Wiliete anaonyeshwa kadi ya njano kwa kumchezea faulo nyota wa Yanga SC

Dakika ya 86 Yanga SC wanapata pigo huru nje kidogo ya 18 linapigwa na Ecua.

Goooooal Yanga SC

Dakika ya 82 Prince Dube anafunga goal la 3 kwa Yanga SC akiwa ndani ya 18

Dakika ya 75 mfungaji wa bao la kwanza kwa Yanga SC, Aziz anatoka nafasi yake inachukuliwa na Conte, Zimbwe Jr naye anaingia akichukua nafasi ya Boka., Duke Abuya anakuwa mchezaji wa kwanza kuonyeshwa kadi ya njano kwenye mchezo wa leo.

Goooooal Yanga SC

Dakika ya 72 Edmund John anafunga goal la pili kwa Yanga SC akitumia pasi ya Maxi Nzengeli

Dakika ya 70 Pacome anakwenda nje nafasi yake inachukuliwa na Celestin Ecua

Dakika ya 69 Yanga SC wanapata kona inapigwa na Pacome

Dakika ya 66 Edmund John anapewa jukumu la kupiga kona iliyosababishwa na beki wa Wiliete baada ya kuokoa krosi iliyopigwa na Boka.

Dakika ya 62 Edmund anafanya jaribio akiwa ndani ya 18 linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete, nyota wawili wa Wiliete ikiwa ni Daniel Nicholas  wanapata maumivu kwenye harakati za kuokoa.

Dakika ya 61 Israel Mwenda anapiga krosi inakutana na Edmund John jaribio lake linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete.

Dakika ya 59, Maxi anaingia anatoka Mzize

Edmund John anaingia anatoka Doumbia

Dakika ya 58 Thobias anapeleka mashambulizi kwa Yanga SC, kiungo mshambuliaji wa Wiliete alifanya jaribio halikuwa na faida.

Dakika ya 55 Djigui Diarra anapeleka mashambulizi mbele na mpira unamfikia Mzize

Dakika ya 50 Wiliete SC wanafanya jaribio ambalo linakwenda nje kidogo ya 18

Dakika ya 48 Thobias anapeleka mashambulizi Yanga SC, Junior anaokoa krosi ya Mwenda na Yanga SC wanapata kona inapigwa na Doumbia inaokolewa na mlinda mlango.

Dakika ya 47 Aziz Andambwile anaanzisha mashambulizi, Doumbia anampa pasi Dube akiwa ndani ya 18 jaribio lake linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete SC.

Kipindi cha pili

Eddy anakwenda benchi kwa Wiliete na dakika 45 zinakwenda kuanza kutoka Angola

Mapumziko

Dakika 45 zimekamilika, Wiliete SC 0-1 Yanga SC, goal kwa Yanga SC limefungwa na Aziz Andambwile akiwa nje ya 18.

Dakika ya 45 Bacca anaokoa hatari, Mzize anapata maumivu

Dakika ya 44 Agustino anaokoa hatari na kuanzisha mashambulizi haraka kuelekea lango la Yanga SC

Dakika ya 42 Pacome anatoa krosi kwa Dube akiwa ndani ya 18 jaribio lake linaokolewa na mlinda mlango wa Wiliete.

Dakika ya 40 Yanga SC wanapata kona, kipa wa Wiliete ameokoa hatari nne ambazo zilikuwa zinakwenda kwenye lango

Dakika ya 39 nahodha wa Wiliete anatoa mpira nje inakuwa kona kwa Yanga SC, Dube anafanya jaribio kwa pigo la kichwa akitumia krosi ya Pacome inaokolewa na mlinda mlango.

Dakika ya 38 Thobias wa Wiliete anaokoa krosi iliyopigwa na Israel Mwenda

Dakika ya 37, Pacome anatoa pasi kwa Dube pembeni inaokolewa

Dakika ya 36 Wiliete wanafanya jaribio kuelekea lango la Yanga SC

Goooal Yanga

Dakika ya 31 Aziz Andambwile anafunga goal kwa Yanga SC akiwa nje ya 18 likimshinda mlinda mlango wa Wiliete SC.

Dakika ya 30 Pacome anatengeneza pasi nzuri ndani ya 18 kwa Wileiete inaokolewa na Jr

Dakika ya 28 pasi ya maelekezo kutoka kwa Doumbia inamkuta Mzize ndani ya 18, anafanya jaribio kwa mguu wake wa kushoto linakwenda nje ya 18

Dakika ya 26 Pacome anapiga krosi kuelekea ndani ya eneo la 18 kwa Wiliete SC inaokolewa

Dakika ya 25 Duke Abuya anachezewa faulo, kipa wa Wiliete SC anawapanga wachezaji wake na nyuma ya mpira yupo Pacome na Doumbia

Dakika ya 21 Prince Dube anafanya jaribio kuelekea Wiliete linaokolewa na kipa wa Wiliete SC

Dakika ya 20 Pacome anafanya jaribio ndani ya 18 linaokolewa na kipa wa Wiliete SC

Dakika ya 19 Yanga SC inapata kona inapigwa na Doumbia, Wiliete SC wanaokoa

Dakika ya 16 Duke Abuya anacheza faulo kwa mchezaji wa Wiliete SC

Dakika ya 13 Yanga SC wanatengeneza nafasi nzuri yakufunga Clement Mzize akiwa ndani ya 18 anakwama kufanya jaribio linakwenda nje ya 18

Dakika ya 12 Aziz Andambwile anampa pasi Nondo ambaye anapeleka mpira mbele , Abuya anacheza faulo kwa nyota wa Wiliete

Dakika ya 11 Agustino kipa wa Wiliete anapeleka mashambulizi mbele

Dakika ya 9 Wiliete wanapata kona ya kwanza iliyosababishwa na Boka, Diarra anaokoa pigo hilo

Dakika ya 7 Bakari Nondo anapeleka mashambulizi mbele ya Wiliete, Clement Mzize anafanya jaribio kwa pigo la kichwa linakwenda nje ya lango

Dakika ya 5 Prince Dube anafanya jaribio ambalo halileti matunda

Dakika ya 4 Clement Mzize anachezewa faulo nje kidogo ya 18

Dakika ya nne Wiliete wanarudisha mpira kwa kipa Agustino Kalougha

Dakika ya tatu Yanga SC wanapiga faulo ya kwanza kupitia kwa Doumbia

Wiliete SC 0-0 Yanga SC, mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika

Ni katika Estadio 11 de Novembro nchini Angola wakicheza na Wiliete Sports Clube.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.