Katika mchezo huo, Simba ilianza kwa kasi na kufunga bao la kwanza dakika ya 7 kupitia Clatous Chama, kabla ya Cheikh Gueye kuongeza la pili dakika ya 26. Chama alifunga bao lake la pili katika mchezo huo dakika ya 34 na kuifanya Simba kwenda mapumziko ikiwa mbele.
Gueye alirejea tena kwenye orodha ya wafungaji dakika ya 69, huku Makgwala akifunga dakika ya 87. Morice alikamilisha ushindi wa Simba kwa bao la dakika ya 90+3.
Mighty Wanderers ilipata bao lake pekee kupitia Kaliati dakika ya 43.

FT: Simba SC 🇹🇿 6-1 🇲🇼 Mighty Wanderers
⚽ 07’ — Chama
⚽ 26’ — Gueye
⚽ 34’ — Chama
⚽ 43’ — Kaliati
⚽ 69’ — Gueye
⚽ 87’ — Makgwala
⚽ 90+3’ — Morice
Agg: Simba SC 7-1 Mighty Wanderers
Baada ya matokeo hayo, Simba SC sasa itakutana na FC de Agosto de Akonibe ya Guinea ya Ikweta katika hatua ya pili ya awali ya CAF Champions League.