Kikosi cha Simba SC dhidi ya Azam FC katika mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB tayari kimetangazwa.
Ni Mzizima Dabi ambao utakwenda kumpata bingwa mpya mara baada ya mabingwa watetezi Yanga SC kuishia hatua ya nusu fainali.
Azam FC waliwaondoa Yanga SC kwa ushindi wa mabao 3-2 katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa. Leo atakwenda kujulikana bingwa.
Kikosi cha Simba SC Kama langoni atakuwa Djibrilla Kassali akisaidiwa na Duchu, Kibabage, Rushine na Ismael Toure.
Wengine wanaoanza kwenye mechi hii itayoanza saa 11 jioni hii ni; Yusuph Kagoma, Libase Gueye, Neo Maema, Elie Mpanzu, Clatous Chama na Anicet Oura hawa watakuwa kikosi cha kwanza.