TETESI za usajili zinasema Barcelona inatarajia kuongeza wachezaji wawili maarufu katika madirisha mawili yajayo ya uhamisho ya kiangazi, Nico Williams mwaka huu na kisha Erling Haaland mwaka 2025.
Barcelona imeonyesha nia ya kuwasajili Erling Haaland na Nico Williams, lakini kuna changamoto kubwa za kifedha na kiutaratibu zinazohusika.
Kwa Erling Haaland, hatua hii inategemea klabu hiyo kutatua matatizo yake ya kifedha na kuandaa ofa ya kuvutia kwa mshambuliaji huyo wa Norway.
Kipengele cha kutolewa Haaland huko Manchester City kitashuka hadi pauni milioni 148.1 mwaka 2025, na kufanya uhamisho kuwa rahisi zaidi wakati huo.
Hata hivyo, kutokana na mahitaji yake ya mshahara mkubwa, bado haijulikani ikiwa Barcelona inaweza kumudu mpango huo kutokana na matatizo yao ya kifedha yanayoendelea.