Home Sports IKIENDI YA KUOKOTA MAOKOTO

IKIENDI YA KUOKOTA MAOKOTO

Hii ni wikiendi ya kuokota maokoto na sehemu pekee ya kupata maokoto hayo ni pale kwenye nyumba ya mabingwa wa kubashiri kampuni ya Meridianbet kupitia michezo itakayokwenda kupigwa wikiendi hii.

Ligi mbalimbali zitarejea leo Jumamosi na kumuwezesha mteja wa Meridianbet kufurahia wikiendi yake, Kwani mabingwa hao wa michezo ya kubashiri wamegawa ODDS KUBWA katika michezo ya leo Jumamosi.

EPL

Katika ligi kuu ya Uingereza leo itapigwa michezo kadhaa ambapo Manchester City wakiwa kwenye mbio za ubingwa watakua nyumbani kumenyana na klabu ya Wolves, Newcastle United leo watakua ugenini kukipiga na klabu ya Burnley, Mchezo mwingine mkali utakua baina ya klabu ya Brentford ambao watakua nyumbani dhidi ya klabu ya Fulham.

LA LIGA

Kunako ligi kuu nchini Hispania pia itapigwa michezo mikali ya ligi hiyo ambapo vinara wa ligi hiyo klabu ya Real Madrid watakua nyumbani kumenyana na klabu ya Cadiz wakati wakihitaji alama nne tu kua mabingwa wa ligi hiyo, Barcelona wao watakua ugenini kumenyana na klabu ya Girona baada ya kupokea kipigo kizito cha mabao manne katika mchezo wa kwanza, Atletico Madrid wao watakua ugenini kukipiga na klabu ya Real Mallorca.

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali ya itakayopigwa katika ligi mbalimbali barani ulaya leo Jumamosi. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

SERIE A

Kunako ligi kuu ya Italia maarufu kama Serie A napo kutapigwa michezo kadhaa leo ya kibabe kabisa, Ambapo mabingwa ambao tayari wameshatangazwa klabu ya Inter Milan itakua ugenini kumenyana na klabu Sassuolo mchezo ambao utakua muhimu sana klabu ya Sassuolo kwani wako chini katika msimamo wa ligi hiyo, Mchezo mwingine utakua baina ya klabu ya Monza ambao watakua nyumbani kukipiga na klabu ya Lazio katika mchezo mkali wa ligi hiyo. 

BUNDESLIGA

Ligi kuu ya Ujerumani nayo itaendelea leo kwa michezo kadhaa kupigwa ambapo klabu ya Bayern Munich watakua ugenini kukipiga na klabu ya Stuttgart mchezo unaotarajiwa kua na ushindani mkubwa kwani timu hizo zinafatana kwenye msimamo wa ligi hiyo, Augsburg watakua nyumbani kuwakaribisha klabu ya Borussia Dortmund

Vilabu hivi vimefanikiwa kukutana mara nne tu kwenye michuano ya ligi ya mabingwa ulaya ambapo klabu ya Borussia Dortmund wakipata ushindi mara moja, Huku klabu ya PSG wao wakipata ushindi mara mbili na mchezo huo ukimalizika kwa sare mara moja.

Previous articlePROMOSHENI YA NON STOP DROP INATOA MKWANJA MREFU |SHIRIKI KWA KUCHEZA KASINO
Next articleISHU YA MKANDAJI KIBU KUIBUKIA YANGA IPO HIVI