Home Sports YANGA HAO ROBO FAINALI

YANGA HAO ROBO FAINALI

MABINGWA watetezi wa CRDB Federation Cup Yanga wamekata tiketi kutinga hatua ya robo fainali kwa ushindi wakiwa ugenini.

Baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma umesoma Dodoma Jiji 0-2 Yanga.

Bao la mapema dakika ya tatu kupitia kwa Emmanuel Martin ambaye alijifunga dakika ya 3 na Clement Mzize dakika ya 66 alipachika bao la pili.

Katika mchezo wa leo Dodoma Jiji walipata penalti dakika ya 52 Idd Kipagwile alikosa baada ya kupaisha pigo hilo.

Aprili 10 2024 imekuwa siku nzuri kazini kwa Yanga na maumivu kwa Dodoma Jiji.

Previous articleKIKOSI CHA YANGA DHIDI YA DODOMA JIJI
Next articleKasino Mtandaoni Yenye Njia Nyingi za Ushindi|81 Crystal Fruits