Home Sports LIGI YA MABINGWA ULAYA MOTO UTAWAKA LEO

LIGI YA MABINGWA ULAYA MOTO UTAWAKA LEO

Kivumbi cha ligi ya mabingwa ulaya kitaendelea leo ambapo itapigwa michezo miwili mikali kwenye michuano hiyo itakayokutanisha vilabu ambavyo vimekua na uzoefu wa michuano hiyo.

Klabu ya Atletico Madrid wao watakua wenyeji kuwakaribisha Borussia Dortmund kutoka kule nchini Ujerumani, Huku Paris Saint German wao watakua nyumbani kupambana na mabingwa mara tano wa michuano hiyo klabu ya Barcelona.

Usiku wa leo klabu ya Paris Saint German itakua nyumbani katika dimba la Parc De Princes kuwakaribisha klabu ya Barcelona katika mchezo wa robo fainali wa ligi ya mabingwa ulaya mkondo wa kwanza.

Paris Saint German mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Ufaransa watakua kwenye mkakati wa kupambana kulitafuta taji lao la ulaya kwa mara ya kwanza kwenye historia ya klabu hiyo, Lakini wakati huohuo wanakutana na Barcelona ambayo ina uzoefu mkubwa kwenye michuano hiyo hivo mchezo huu unatarajiwa kua mkali kwelikweli.

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali itakayopigwa leo kwenye ligi ya mabingwa barani ulaya. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Kipute kingine kitapigwa pale katika dimba la Wanda Metropolitano ambapo klabu ya Atletico de Madrid itaikaribisha klabu ya Borussia Dortmund kutoka kule nchini Ujerumani, Huku mchezo huo ukitarajiwa kua wenye ushindani mkubwa baina ya vilabu hivyo.

Atletico Madrid wamekua kwenye ubora mkubwa wakifanikiwa kumtoa mwanafainali wa michuano iliyopita klabu ya Inter Milan ya nchini Italia huku wakipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika mchezo huo, Lakini Dortmund ni moja ya vilabu ambavyo vimekua vikifanya vizuri linapokuja michuano ya ulaya.

Michezo yote ya leo inapatikana pale Meridianbet na imepewa ODDS KUBWA ambazo zinaweza kukufanya ukaibuka na mkwanja wa kutosha, cha kufanya ni wewe kutengeneza mkeka wako kupitia michezo hii ya kukata na shoka uweze kupiga mkwanja.

Previous articleSIMBA YAWAFUATA IHEFU SINGIDA
Next articleUTACHEKA HII NA UTAIPENDA: ALI KAMWE NA AHMED ALLY USO KWA USO