UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kuwa mpango mkubwa ni kufanya vizuri kwenye mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Machi 30 2024. Ali Kamwe, Ofisa Habari wa Yanga ameweka wazi kuhusu kuelekea kwenye mchezo huo.