IVORY COAST NA MAAJABU YAO AFCON

IVORY Coast ni mabingwa ushindi wapya wakionyesha maajabu yao kwa kupindua meza kibabe kwenye mchezo wa fainali uliokuwa ni wa kuvuja jasho na akili nyingi.

Baada ya dakika 90 wenyeji Ivory Coast waliibuka kwa ushindi wa mabao 2-1 Nigeria katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2023.

Ikumbukwe kwamba mabingwa watetezi walikuwa nj Senegal waliokwama kutetea taji hilo Ivory Coast.

Mabao ya Ivory Coast ambayo ilipenya ikiwa ni best looser iliwashangaza Nigeria kwa mabao ya Frank Kessie dakika ya 62 na la ushindi lilifungwa na Sebastien Haller dakika ya 81.

Ivory Coast mabingwa AFCON 2023 ikiwa ni mara ya tatu kutwaa taji hilo kubwa Afrika.

Licha ya nyota Ekong mapema kuwatanguliza Nigeria dakika ya 37 halikutosha kuwapa taji hilo katika mchezo wa fainali iliyokuwa na ushindani mkubwa ñdani ya uwanja.

Ilikuwa kazi kubwa na mwisho imehitimshwa huku Afrik Kusini wakiwa ni washindi watatu kwenye AFCON hiyo.