HIVI HAPA VIGONGO VYA SIMBA NDANI YA FEBRUARI

NDANI ya Februari kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Abdelhak Benchikha kina kazi kubwa ya kusaka pointi tatu ambazo wapinzani wao wanazihitaji pia.

Kigongo cha kwanza kinatarajiwa kuwa leo Februari 3 ugenini mwisho wa reli Kigoma kwa kupambana dhidi ya wenyeji wao Mashujaa Uwanja wa Lake Tanganyika.

Katika mchezo wa leo Simba imemuongeza kiungo Clatous Chama ambaye alikuwa nje kwa muda mrefu kutokana na adhabu ambayo alikuwa nayo kwa sasa akiwa amesamehewa.

Mashujaa v Simba Februari 3

Tabora United v Simba, Februari 6

Simba v Azam FC Februari 9

Geita Gold v Simba, Februari 12

JKT Tanzania v Simba, Februari 15

Simba v Mtibwa Sugar, Februari 18