BOSI WA MAN CITY ATIMKIA MAN UTD KUWA CEO MPYA

Manchester United imemteua aliyekuwa CEO wa Man City, Omar Berrada kuwa Afisa Mtendaji Mkuu mpya klabuni hapo akichukua mikoba ya Richard Arnold aliyebwaga manyanga baada ujio wa Sir Jim Ratcliffe.

Ujio wa Berrada Manchester United ni pigo kwa upande wa pili wa Manchester ikizingatiwa Mhispania huyo amefanya kazi kwa karibu na Pep Guardiola na amekuwa Mkuu wa Uendeshaji wa klabu ya Manchester City.

Taarifa ya Manchester City juu ya kuondoka kwa Berrada imesema : “Klabu ya Manchester City inaweza kuthibitisha kwamba Omar Berrada amejiuzulu kama afisa mkuu wa uendeshaji wa soka katika ‘City Football Group’.