AZAM FC WAKOMBA POINTI MKWAKWANI, FEI AWAKA
WAKIWA ugenini, Azam FC imekomba pointi tatu mazima dhidi ya Coastal Union kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Bao la ushindi limefungwa na Feisal Salum, dakika ya 45 kwa pigo akiwa ndani ya 18 kutokana na makosa ya safu ya ulinzi ya Coastal Union. Ni bao la nne kwa Fei Toto ambaye alifungua akaunti…