Kikosi cha Timu ya Soka ya Wanawake ya Simba Queens kimefanikiwa kuingia Fainali ya Ngao ya Jamii Wanawake 2023 kwa kuifunga Yanga Princess kwa penati 5-4 katika Nusu Fainali iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam
Timu hizo zilifika hatua hiyo baada ya matokeo ya 0-0 katika muda wa kawaida, hivyo Simba Queens itavaana na JKT Queens katika Fainali baada ya kuingia hatua hiyo kwa ushindi wa magoli 5-0 dhidi ya Fountain Gate Princess