KIUNGO mzawa Mudathir Yahya anayekipiga ndani ya Yanga ni shujaa chini ya Miguel Gamondi kutokana na uwezo wake kila anapopata nafasi.
Nyota huyo kwenye mchezo dhidi ya Namungo FC uliochezwa Uwanja wa Azam Complex alionyesha mekeke yake alipotokea benchi.
Baada ya dakika 90 kwenye mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa ubao ulisoma Yanga 1-0 Namungo FC na mtupiaji alikuwa Mudhathir.
Bao hilo la kwanza lilipachikwa dakika ya 87 ikiwa imebaki dakika chache mchezo kugota mwisho.
Ushindi huo unaipa Yanga pointi tatu wakiwa namba moja kwenye ligi na pointi zao kibindoni ni 9 baada ya kucheza mechi tatu na hawajapoteza mchezo ndani ya ligi.
Tottenham Hotspur forward Dominic Solanke battles with Crystal Palace defender Maxence Lacroix during the English championship Premier League football match between Crystal Palace and Tottenham Hotspur on 27 October 2024 at Selhurst Park in London, England - Photo Ian Stephen / ProSportsImages / DPPI (Photo by IAN STEPHEN / ProSportsImages / DPPI via AFP)