IMEELEZWA kuwa winga Leandre Onana mwenye miaka 23 mali ya Rayon Sports ya Rwanda yupo kwenye hesabu za mabosi wa Simba.
Timu hiyo imekosa taji la Ligi Kuu Bara ambao upo mikononi mwa Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi.
Nyota huyo ni winga ametupia mabao 15 na pasi 10 za mabao ametoa ndani ya timu hiyo.
Yote hayo ni katika Ligi Kuu ya Rwanda anatajwa kuwa kwenye rada za timu za Simba inayopambana kuboresha kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu Roberto Oliveira.