KUELEKEA kwenye mchezo wa kesho wa Ligi Kuu Bara kati ya Dodoma Jiji dhidi ya Simba, nyota wa timu hiyo Clatoous Chama hatakuwa sehemu ya kikosi.
Chama ni namba moja kwenye kutengeneza pasi za mabao akiwa ametoa asi 12 na kufunga mabao matatu.
Kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Mbeya City nyota huyo alitoa pasi moja ya bao kwa mshikaji wake Saidi Ntibanzokiza ambaye alipachika bao hilo dakika ya 19.
Kwa mujibu wa Juma Mgunda, kocha msaidizi wa Simba amesema kuwa Chama kwenye mchezo dhidi ya Mbeya City alikuwa anacheza akiwa anasumbuliwa na Malaria pamoja na mafua.
Alipoyeyusha dakika 33 benchi la ufundi likaona inatosha na hayupo kwenye msafara wa Simba uliopo kwa wakulima Zabibu, Dodoma.