Home Uncategorized SIMBA MATUMAINI MAKUBWA KUFANYA VIZURI

SIMBA MATUMAINI MAKUBWA KUFANYA VIZURI

JUMA Mgunda, Kocha Mkuu wa Simba amesema ushindi wao mbele ya Eagle unawapa nguvu ya kuzidi kuimarika kwa mechi zijazo.

Ikiwa Uwanja wa Mkapa, Desemba 10, ubao ulisoma Simba 8-0 Eagle na timu hiyo ikatinga hatua ya 32 Kombe la Shirikisho.

“Tumekuwa na mwanzo mzuri na hii inatupa nguvu kwa ajili ya mechi zijazo kufanya vizuri na inawezekana kutokana na namna wachezaji ambavyo wanajituma.

“Makosa ambayo yametokea hayo ni sehemu ambayo tutafanyia kazi kwenye uwanja wa mazoezi kikubwa ni kuzidi kuwa kwenye mwendelezo mzuri,” amesema

Kwenye mchezo huo nyota wa Simba, Habib Kyombo alifungua pazia la mabao huku Moses Phiri akitupia mabao manne, Clatous Chama mawili na Sakho bao moja.

Previous articleMABINGWA WATETEZI KUTUPA KETE YAO KWA MKAPA
Next articleYANGA YACHAPA MTU BAO 8-0 KWA MKAPA