Home International GHANA HAWANA BAHATI NA PENALTI KOMBE LA DUNIA

GHANA HAWANA BAHATI NA PENALTI KOMBE LA DUNIA

TIMU ya taifa ya Ghana kwenye Kombe la Dunia tangu mwaka 1966 wakati rekodi zinatajwa kuanza kukusanywa inakuwa timu ya kwanza kukosa penalti mara mbili kwa timu moja.

Ilikuwa ni mwaka 2010 na 2022 mbele ya timu ya taifa ya Uruguay jambo ambalo linawasumbua kwa kweli Waafrika hawa.

Wakati wakifungwa mabao 2-0 dhidi ya Uruguay kwenye mchezo wa makundi ni staa wao Andre Ayew alikosa penalti.

Licha ya kufungwa na Uruguay kushinda wote wameondolewa kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2022 Qatar kutoka kundi H baada ya Korea Kusini kufanya maajabu na kushinda mchezo wao.

Previous articleUTAMU WA KOMBE LA DUNIA HATUA YA 16 BORA KITAWAKA, PATA MACHAGUO SPESHO
Next articleNYOTA HAWA SIMBA KUPIGWA PANGA