Home International MASTAA WAWILI CITY WAFUNGA TATUTATU DHIDI YA MAN U

MASTAA WAWILI CITY WAFUNGA TATUTATU DHIDI YA MAN U

UWANJA wa Etihad kwenye mchezo wa Ligi Kuu England mastaa wawili wa Klabu ya Manchester City wamefunga hat trick ikiwa ni Erling Haaland aliyetupia dakika ya 34,44,65.

Kwenye mchezo huo baada ya dakika 90 ubao ulisoma Manchester City 6-3 Manchester United ikiwa ni dabi iliyokusanya mabao 9 baada ya mchezo huo kukamilika.

Staa mwingine wa City ambaye ametupia ni Phil Foden dakika ya 8,44 na 64 kwenye mchezo huo.

Kwa United ni bao la Antony lilianza kuwa la ufunguzi kwao dakika ya 56 kisha dakika ya 84 na 90+1 lilipachikwa bao la tatu na yote mawili yalifungwa na Anthony Martial.

Ni pointi 20 wanafikisha City wakiwa nafasi ya pili namba moja ni Arsenal wenye pointi 21 wote wakiwa huku United ikiwa nafasi ya 6 na pointi 12 kwenye msimamo

Previous articleSIMBA YAICHAPA TATU DODOMA JIJI NA KUSEPA NA POINTI TATU
Next articleMAAJABU YA MGUNDA SIMBA, YANGA V RUVU LITAKUFA JITU