Home International RB LEIPZIG YAPIGWA 3-0 BUNDESLIGA

RB LEIPZIG YAPIGWA 3-0 BUNDESLIGA

BUNDESLIGA moto unawaka baada ya Klabu ya Monchengladbah kuishushia kichapo cha mabao 3-0 RB Leipzig.

Katika mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Borussia Park staa wao Janas Hofmann alitupia mabao mawili dakika ya 10 na 35.

Bao lingine lilijazwa kimiani na Ramy ensebaini ilikuwa dakika ya 53 lilifunga ukurasa wa pointi tatu jumlajumla.

Ni mashuti 21, Monchengladbah walipiga huku 10 yakilenga lango na RB Leipzing wao walipiga mashuti 12 na mashuti matano yalilenga lango.

Kwenye msimamo Monchengladbah ipo nafasi ya 6 na pointi 12 huku RB Leipzing ikiwa nafasi ya 12 na pointi 8.

Previous articleVIDEO:KOCHA BIG BULLETS AWAONYA SIMBA
Next articleSIMBA YASONGA MBELE KIMATAIFA, PHIRI KAWA MCHARO