Home Sports MAPUMZIKO:SIMBA 1-0 ST GEORGE Sports MAPUMZIKO:SIMBA 1-0 ST GEORGE August 8, 2022 FacebookTwitterPinterestWhatsApp UWANJA wa Mkapa, mchezo wa kirafiki ni mapumziko, Simba 1-0 Saint George SC mtupiaji ni Kibu Denis. Mzawa huyo ametupia bao hilo kwa shuti kali akitumia mguu wake wa kulia lililomshinda mlinda mlango wa St.George. Leo ni kielel cha Simba Day ambapo kuna burudani zinaendelea Uwanja wa Mkapa. Pia mastaa wa Simba ikiwa ni pamoja na Meddie Kagere,Taddeo Lwanga ambao wameweka wazi kuwa walikuwa na muda mzuri ndani ya Simba. Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano,Ahmed Ally ameweka wazi kuwa jambo ambalo wanahitaji kwa msimu wa 2022/23 ni mataji. “Ambacho tunahitaji kwa msimu mpya ni kushinda ubingwa na mashabiki nao wanazungumza kuhusu hili moja kwa moja na wachezaji,”.