Home International SIMBA NDANI YA BERKANE

SIMBA NDANI YA BERKANE

KIKOSI cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Pablo Franco leo Februari 26 kimewasili salama mji wa Berkane.

Safari ya kuibukia Berkane ilianza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mohammed V uliopo Casablanca.

Simba ina kibarua cha kumenyana na Klabu ya RS Berkane katika mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya makundi, kesho Februari 27.

Ni katika kundi D ambalo vinara ni Simba wakiwa na pointi 4 wanakutana na RS Berkane wenye pointi tatu mchezo wao uliopita walipoteza mbele ya ASEC Mimosas Februari 20 kwa kufungwa mabao 3-1.

Simba imetoka kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya USGN ya Niger.

Previous articleMUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMAMOSI
Next articlePOLISI TANZANIA KUKIWASHA LEO AZAM COMPLEX V KMC