UWANJA WA SOKOINE, MBEYA CITY 1-0 SIMBA

MPAKA muda wa mapumziko, Uwanja wa Sokoine Simba wanatafuta bao la kusawazisha.

Ni Paul Nonga amepachika bao la kuongoza kwa Mbeya City akitumia makosa ya mabeki wa Simba chini ya Inonga Banka.

Lakinj Mbeya City wamekamilisha dakika 45 wakiwa pungufu kwa sababu nyota wao Mpoki Mwakinyuke alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 43.

Sababu ya kwanza ilikuwa kupoteza muda baada ya kuwa mbele kwa bao moja na ya pili ilikuwa ni kumchezea faulo Chris Mugalu.