Home Sports MASTAA YANGA WAPIGWA MKWARA NA MTUNISSIA

MASTAA YANGA WAPIGWA MKWARA NA MTUNISSIA

NASREDDINE Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga ameweka wazi kwamba hakuna mchezaji mkubwa ndani ya kikosi cha Yanga kwa kuwa Yanga ni kubwa kuliko yoyote.
Kocha huyo raia wa Tunissia ameongeza kuwa kuhusu kuanza kikosi cha kwanza kwa wachezaji wake itategemea na namna hali itakavyokuwa kutokana na mchezo husika na haina maana kwamba kufunga mabao ni sababu ya kuweza kuanza kikosi cha kwanza.
Ikumbukwe kwamba nyota wake Heritier Makambo kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Ihefu FC uliochezwa Uwanja wa Mkapa aliweza kufunga mabao matatu lakini Nabi amebainisha kwamba hawezi kuwa na uhakika wa kuanza kikosi cha kwanza.
“Kila mchezaji ndani ya Yanga ni muhimu na ipo wazi kwamba Yanga ni kubwa kuliko mchezaji hivyo haina maana kwamba kufunga ama kutofunga ni sababu za mchezaji kuanza kikosi cha kwanza.
Yanga ipo nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 20 baada ya kucheza mechi nane mchezo wao ujao ni dhidi ya Tanzania Prisons, Uwanja wa Nelson Mandela itakuwa ni Desemba 19.
Previous articleMUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA
Next articleRATIBA YA LIGI KUU BARA LEO DESEMBA 17