MTENDAJI Mkuu wa Bodi ya Ligi TPLB, Almasi Kasongo leo Juni 28, 2022 ametangaza ratiba ya mchezo wa Ngao ya hisani kuwa utachezwa Agosti 13, 2022 mwaka huu.
Kasongo amefafanua zaidi kwa kusema kikanuni mchezo huo hukutanisha bingwa wa ligi na bingwa wa FA, lakini iwapo bingwa wa ligi na FA akiwa ni mmoja basi mchezo huo uta wakutanisha mshindi wa ligi na aliyemaliza nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.