KOCHA ITALIA HAJAFURAHISHWA NA MATOKEO MABAYA

ROBERTO Mancini, Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Italia amesema kuwa hajafurahishwa  na kutolewa katika hatua hiyo.

Usiku wa kuamikia leo Timu ya Taifa ya Italia ilifungwa bao 1-0 dhidi ya North Macedonia.

Bao pekee la ushindi lilipachikwa kimiani na Aleksandar Trajkovski dk 90+2 Uwanja wa Renzo Barbera.

Sasa North Macedonia itacheza mchezo dhidi ya Ureno ili kuweza kukata tiketi ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia.

Mancini amesema:”Kwa kilichotokea sijapenda na siwezi kuzungumza juu ya mambo ya wakati ujao,”.