Leo Juni 6, 2026 saa 20:45 usiku Uwanja wa Estádio Nacional huko Jamor, Oeiras (karibu na Lisbon) utakuwa jukwaa la mchezo wa kirafiki kati ya Portugal na Chile.
Kwa Portugal ambao wamepangwa Kundi K la Kombe la Dunia 2026 pamoja na Kolombia, Uzbekistan na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, huu ni mchezo wao wa mwisho kabla ya safari ya Amerika Kaskazini, huku Chile wakitumia fursa hii kujenga msingi wa kizazi kipya baada ya kukosa tiketi ya kufuzu.
Katika historia timu hizi zimekutana mara tatu, zote zikiwa sare katika muda wa kawaida. Mechi ya kukumbukwa zaidi ilikuwa Juni 28, 2017 kwenye Kombe la Mashirikisho, ambako Chile iliibuka washindi kwa penalti 3-0 baada ya muda wa kawaida na nyongeza kumalizika 0-0. Mechi ya awali iliyochezwa mwaka 2011 nchini Ureno ilimalizika kwa sare ya 1-1. Bado hakuna timu iliyowahi kumaliza mchezo wa kawaida ikiwa mshindi dhidi ya nyingine.
Kocha wa Portugal Roberto Martínez yuko katika mchakato wa kuiakifisha timu yake, ingawa amekosa wachezaji wanne muhimu waliocheza fainali ya Ligi ya Mabingwa mwishoni mwa wiki Vitinha, Nuno Mendes, João Neves na Gonçalo Ramos wa PSG. ambao watajiunga na kikosi baada ya mechi hii. Cristiano Ronaldo anatarajiwa kuwa kwenye safu ya ushambuliaji, akisaidiwa na Bruno Fernandes na Bernardo Silva wanaotarajiwa kuendesha mashambulizi ya Ureno. Kipa Ricardo Velho ameahidi timu iko tayari kwa changamoto yoyote.
Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.
Upande mwingine, Chile inaongozwa na kocha wa muda Nicolás Córdova ambaye ameitisha kikosi chenye mabadiliko makubwa. “Generación Dorada” ya Alexis Sánchez na Arturo Vidal haipo, wakati mabadiliko yanaonekana katika kila safu. Lawrence Vigouroux anatazamiwa kuanza kwenye lango, huku nahodha Gabriel Suazo wa Sevilla akiongoza safu ya ulinzi. Darío Osorio na Lucas Cepeda wanategemewa kuleta kasi katika ushambuliaji, huku kiungo mwenye asili ya Uswisi Nils Reichmuth akiwa mgeni rasmi katika kikosi cha taifa.
Estádio Nacional unatazamiwa kujaa mashabiki zaidi ya 35,000, na Portugal wakiwa na rekodi ya ushindi 11 mfululizo katika mechi za nyumbani. Wachambuzi wanatabiri ushindi wa Portugal kutokana na ubora wa wachezaji wao, huku Chile wakiwa katika mchakato wa kujenga timu.
Mchezo huu utakuwa jaribio la mwisho kwa timu zote Portugal kabla ya kukutana na Nigeria Juni 10 kisha kuelekea Marekani, huku Chile wakifuatia mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Juni 9 mjini Hispania.