CRDB Cup ni hatua ya robo fainali ambapo timu zinatarajiwa kushuka uwanjani kusaka ushindi kutinga hatua ya nusu fainali.
Haya ni mashindano mengine makubwa Bongo ambapo ni hatua ya mtoano mpaka fainali ukishinda unasonga mbele ukifungwa umeumaliza mwendo.
Katika mashindano haya ambayo yapo hatua ya robo fainali mabingwa watetezi ni Yanga SC watakuwa kazini Mei 16 kusaka nafasi kutinga hatua ya nusu fainali.
Mei 16, 2026 ni Coastal Union vs Singida Black Stars, saa 10:00 jioni, JKT Tanzania vs Yanga SC, saa 12:30, Jumapili Mei 17 zitapigwa mechi mbili kali pia.
Mashujaa FC vs Azam FC saa 10:00 jioni, Simba SC vs TRA United, saa 12:30, washindi kwenye kila mechi watasonga mbele hatua ya nusu fainali.