Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Yashika Nafasi ya 6 Afrika, Yapanda hadi Nafasi ya 54 Duniani

Kwa mujibu wa takwimu zilizotangazwa juma hili,Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara inashika nafasi ya sita (6) kwa ubora barani Afrika na ya 54 duniani.

Licha ya kushuka kwa nafasi mbili (2) Afrika ikilinganishwa na mwaka 2024, Ligi yetu imepanda kwa nafasi tatu (3) duniani, kutoka nafasi ya 57 (2024) hadi nafasi ya 54 (2025) na alama zimeongezeka kutoka 266.75 (2024) hadi 308.5 (2025).

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania imewashukuru wadau wote wa Ligi hii kwa jitihada zilizofanya Ligi yetu iendelee kuwa miongoni mwa Ligi Bora na zenye mvuto barani Afrika.