Bao la dakika za jiooonia John Stones limeipatia Manchester City alama zote dhidi ya Wolverhampton katika dimba la Molineux kwenye mchezo wa Ligi Kuu England.
Wolves 1-2. Man City
⚽ 7’ Larsen
⚽ 33’ Gvardiol
⚽ 90+5’ Stones
Manchester City imekwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu England ikifikisha pointi 20 baada ya mechi 8 ingawa inaweza isidumu kwa muda mrefu kwenye nafasi hiyo ikiwa Liverpool watashinda dhidi ya Chelsea muda mfupi ujao.