SIMBA YATAMBULISHA UZI MPYA MKALI

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba leo Januari 3 2022 wametambulisha uzi mpya.

Ni uzi maalumu ambao utatumika katika Kombe la Shirikisho pamoja na Kombe la Mapinduzi ambalo linafanyika Zanzibar.

Tayari kikosi kimewasili Zanzibar kwa ajili ya mashindano hayo ambayo yameanza kurindima jana Januari 2.

Mchezo wao wa kwanza unatarajiwa kuwa ni Januari 5,2022 dhidi ya Selem View.