>

AZAM YATANGAZA KUACHANA NA NYOTA WAKE WANNE

Klabu ya Azam FC imetangaza kuachana na nyota wake WANNE ambao ni pamoja na Ayoub Lyanga, Edward Manyama, Malickou Ndoye na Issa Ndala ambao mikataba yao klabuni hapo imefikia ukomo.

Taarifa ya Azam Fc kwenye mitandao ya kijamii imesema: “Ahsanteni sana kwa mchango wenu wa kuipigania nembo ya klabu yetu kwa kipindi chote mlichokuwa nasi. Tunawatakia kila la kheri huko muendako katika safari yenu nyingine ya soka.”