KIKOSI cha Simba kinatarajiwa kuwa uwanjani leo kwenye msako wa pointi tatu dhidi ya Namungo, Aprili 30 2024.
Ikumbukwe kwamba katika mchezo wa mzunguko wa kwanza walipokutana Uwanja wa Uhuru ubao ulisoma Simba 1-1 Namungo FC walipogawana pointi mojamoja.
Mchezo uliopita kwa Simba ambao ulikuwa ni wa mwisho kwa Abdelhakh Benchikha kukaa benchi ilikuwa Aprili 20 2024 alishuhudia ubao ukisoma Yanga 2-1 Simba.
Leo kikosi cha Simba kipo mikononi mwa Juma Mgunda akishirikiana na Seleman Matola.
Kuna nyota ambao watakosekana ambao ni Clatous Chama, Luis Miqussone, Shomari Kapombe kwa kuwa bado hawajawa fiti.