Home Sports FAINALI MUUNGANO SIMBA V AZAM FC

FAINALI MUUNGANO SIMBA V AZAM FC

BAADA ya Azam FC kupata ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya KMKM kwenye mchezo wa nusu fainali ya Muugano sasa inakwenda hatua ya fainali itakutana na Simba.

Aprili 25 ubao wa Uwanja wa New Amaan Complex baada ya dakika 90 ulisoma Azam FC 5-2 KMkm kwenye nusu fainali ya pili.

Mchezo wa fainali unatarajiwa kuchezwa Aprili 27 kwa wababe hao kusaka bingwa mpya wa 2024.

Ikumbukwe kwamba Simba ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya KVZ ambapo mwamba Michel Fred alipachika bao la ufunguzi na bao la pili ni mali ya Israel Mwenda kwa mkwaju wa penalti.

Previous articleORB OF DESTINY KUTOKA MERIDIANBET KASINO NJIA 14 ZA MALIPO
Next articleYANGA YAVUTA WATANO, MIKATABA MASTAA SIMBA YACHANWA