KWENYE msako wa kuwania tuzo ya mchezaji bora ndani ya kikosi cha Yanga Oktoba ni Stephane Aziz Ki ameshinda tuzo hiyo.
Kiungo huyo raia wa Burkina Faso alikuwa akiwania tuzo hiyo na nyota wengine wawili aliongia nao fainali.
Ni beki wa kazi Dickson Job na Max Nzengeli ambao walichaguliwa kuwania tuzo hiyo.
Aziz Ki atazawadiwa kiasi cha shilingi milioni 4 na tuzo kama ilivyobainishwa awali na mdhamini wa tuzo hiyo ambaye ni Kampuni ya NIC Insurance.