Home Uncategorized NMB YADHAMINI MASHINDANO YA GOFU

NMB YADHAMINI MASHINDANO YA GOFU

BENKI ya NMB Tanzania imeweka wazi kuwa sababu kubwa ya kuendelea kuwa karibu na Watanzania wengi zaidi wameamua kuendeleza mpango wao wa kudhamini mashindano ya Gofu Tanzania.

Taarifa kutoka NMB imeeleza kuwa kwa kutambua umuhimu wa michezo kwenye jamii, NMB inaendelea kuwa wadhamini wakuu wa mashindano ya Gofu ya Mkuu wa Majeshi kwa mwaka 2023.

Mashindano hayo kwa 2023 yanatarajiwa kufanyika  Lugalo Golf Club, Septemba 2 na 3.

Huu unakuwa ni mwaka wa 8 kwa NMB kudhamini mashindano hayo, huku wakiwa na lengo la kuhakikisha wanawafikia Watanzania wengi zaidi kulingana na michezo wanayopenda.

Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi  Aikansia Muro amekabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni 30 kwa Mwenyekiti wa Klabu ya Gofu ya Lugalo  Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo ikiwa ni udhamini wa mwaka huu.

Makabidhiano hayo yalishuhudiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Gofu Tanzania (TGU), Gilman Kasiga, Kapteni wa Klabu ya Gofu ya Lugalo, Meja Japhet Masai na Meneja Mwandamizi wa Idara ya Wateja Binafsi, Priscus Kavishe.

Previous articleAZAM FC KWENYE KISASI KIMATAIFA
Next articleYANGA NA SIMBA KILA UPANDE UMETOA TAARIFA LAKINI BADO