Home Sports TUZO YA AZAM SPORTS FEDERATION SIMBA HAWAJAPENYA Sports TUZO YA AZAM SPORTS FEDERATION SIMBA HAWAJAPENYA May 20, 2023 FacebookTwitterPinterestWhatsApp KAMATI ya Tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzaniam (TFF) imefanya uteuzi wa washiriki katika makundi mbalimbali ya Tuzo hizo. Ni makundi matano ambayo ni Tuzo ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports Federation Tuzo za Ligi Kuu ya Wanawake Tuzo za Ligi Kuu Bara Tuzo za Utawala Tuzo za Ligi nyingine Hizi ni Tuzo za Kombe la Shirikisho Kipa Bora Benedick Haule wa Singida Big Stars Djigui Diarra wa Yanga Abdulai Idrissu wa Azam FC Mchezaji Bora Taarifa imeeleza kuwa wateule watatangazwa Mei 21 baada ya mechi ya nusu fainali ya pili kati ya Singida Big Stars dhidi ya Yanga Mfungaji bora ambapo mshindi ni yule atakayekuwa amefunga mabao mengi Andrew Simchimba wa Ihefu katupia mabao 7 lakini timu hiyo imeondolewa kwenye mashindano ila mabao hayajafutwa Clement Mzize wa Yanga katupia mabao sita Abdul Suleiman wa Azam katupia mabao matatu. Katika orodha hii hakuna nyota kutoka kikosi cha Simba ambaye amepenya .