Home Sports HUU HAPA MTAMBO WA MABAO MTIBWA SUGAR

HUU HAPA MTAMBO WA MABAO MTIBWA SUGAR

NDANI ya Ligi Kuu Bara mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Charles Ilanfya ametupia mabao manne akiwa ni namba moja kwa utupiaji kwenye kikosi hicho kilicho nafasi ya 12 na pointi 29.

Ikumbukwe kwamba kinara wa utupiaji anatokea ndani ya Yanga ambaye ni Fiston Mayele mwenye mabao 16.

Ni mabao 27 safu ya ushambuliaji ya Mtibwa Sugar imefunga msimu huu wa 2022/23.

Timu hiyo mchezo wake uliopita ilipoteza kwa kushuhudia ubao wa Uwanja wa Mkwakwani Tanga ukisoma Coastal Union 1-0 Mtibwa Sugar.

Ilikuwa ni Aprili 23 2023 walipopoteza pointi tatu muhimu ambazo zinawafanya wabakie na pointi zao 29 huku Coastal Union wakifikisha pointi 30 nafasi ya 11.

Kituo kinachofuata kwa Mtibwa Sugar ni Mei 15 dhidi ya Polisi Tanzania mchezo unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa manungu.

Previous articleVIDEO:YANGA YAWEKA VIZUIZI KESI YA FEI,KESI IMESHAFUNGWA
Next articleMANCHESTER UNITED WAPOTEZA POINTI JIONI