Home Sports POLISI TANZANIA YAPANDA NAFASI MOJA

POLISI TANZANIA YAPANDA NAFASI MOJA

USHINDI ambao wameupata Polisi Tanzania kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ihefu umewaondoa kutoka nafasi ya 16 mpaka 15.

Katika mchezo uliochezwa Aprili 21 baada ya dakika 90 ubao ulisoma Polisi Tanzania 2-1 Ihefu.

Mabao ya Ihefu yalifungwa na Kelvin Sabato huku lile la Ihefu likifungwa na Adam Adam.

Ushindi huo unaifanya Polisi Tanzania kufikisha jumla ya pointi 22 baada ya kucheza mechi 27 huku Ruvu Shooting ikiwa na pointi 20.

Sasa ni Ruvu Shooting ya Kibaha ipo nafasi ya 16 na pointi 20 leo ina kibarua cha kusaka pointi tatu dhidi ya Azam FC, Uwanja wa Jamhuri,Moro.

Previous articleSIMBA 1-0 WYDAD CASABLANCA
Next articleSIMBA YAIBUKA NA USHINDI DHIDI YA WYDAD