Home Sports KIPA SIMBA SC AINGIA ANGA ZA AZAM FC

KIPA SIMBA SC AINGIA ANGA ZA AZAM FC

INAELEZWA kuwa Klabu ya Azam FC ipo kwenye hesabu za kuinasa saini ya kipa namba mbili wa Simba, Beno Kakolanya.

Mkataba wa kipa huyo ambaye aliongeza hivi karibuni miaka miwili unatarajiwa kugota ukingoni hivi karibuni.

Taarifa inaeleza kuwa Beno ameahidiwa mshahara mkubwa zaidi ya anaolipwa ndani ya Klabu ya Simba pamoja na uhakika wa kuanza ndani ya kikosi cha kwanza cha Azam endapo atajiunga nao.

Kwa sasa timu hiyo kipa wake namba moja ni Ali Ahamada ambaye ameanza kikosi cha kwanza kwenye mechi 14 msimu wa 2022/23.

Previous articleSIMBA YAKUSANYA FURUSHI LA POINTI KANDA YA ZIWA
Next articleKARIBU KWENYE FAMILIA YA KIBINGWA YA MERIDIANBET UFURAHIE SLOTI YA BURSTING HOT 5