Home Uncategorized HAWA HAPA WAPINZANI WA SIMBA KOMBE LA SHIRIKISHO

HAWA HAPA WAPINZANI WA SIMBA KOMBE LA SHIRIKISHO

KWENYE droo ya Azam Sports Federation raundi ya pili ambayo imechezwa leo Novemba 30,2022 Simba imewatambua wapinzani wake.

Ni kikosi cha Eagle kitapambana na Simba kusaka ushindi kwenye mchezo wao huo ujao.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kati ya Desemba 9-11, 2022 ambapo Simba waliweka wazi kuwa wanahitaji kutwaa taji hilo.

Mabingwa watetezi wa taji hilo ni Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi raia wa Tunissia.

Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano ndani ya Simba, Ahmed Ally ameweka wazi kuwa malengo ya timu hiyo ni kupata matokeo kwenye mechi zote wanazocheza.

“Kwenye kila mechi ambazo tunacheza kikubwa ni kupata matokeo iwe ni ligi ama Kombe la Shirikisho,wachezaji wanajua kwamba kila mmoja anafanya kazi kubwa kwenye kusaka ushindi,”.

Previous articleKOMBE LA DUNIA 2022: SENEGAL IMEKUWA NCHI YA KWANZA YA AFRIKA KUVUKA NGAZI YA MAKUNDI
Next articleMABINGWA WA KOMBE LA SHIRIKISHO KUANZA NA KURUGENZI