HALI ilikuwa mbaya kwa Barcelona kwenye mchezo wa UEFA Champions League ndani ya dakika 90 kwa kuwa hakuna shuti hata moja walilopiga likalenga lango.
Katika mashuti 9 waliyopiga ilikuwa ngumu kupenya kwenye ngome ya Bayer ya Msenegal Sadio Mane ambaye alianza kuwatungua dakika ya 10 kwenye mchezo huo.
Licha ya kuwa walikuwa Uwanja wa Camp Nou walishuhudia wakichapwa mabao 3-0 na kuwafanya wabaki na pointi zao 4 wakiwa nafasi ya tatu kwenye kundi C baada ya kucheza mechi tano.
Mabao mengine yalifungwa na Eric Maxim Choupo-Moting dakika ya 31 na lile la tatu lilijazwa kimiani na Banjamin Parard dakika 90+5 na kuwafanya wawe nafasi ya kwanza na pointi 15.
Team Canada forward Jonathan David (#7) watches as his shot is saved by the Iceland goalkeeper during an international friendly match between Canada and Iceland at BMO Field in Toronto, Ontario, Canada, on March 28, 2026. (Photo by Indrawan Kumala/NurPhoto) (Photo by Indrawan Kumala / NurPhoto via AFP)