Home Sports FT:YANGA 2-1 SIMBA UWANJA WA MKAPA

FT:YANGA 2-1 SIMBA UWANJA WA MKAPA

YANGA imeanza kwa kutetea taji lao la Ngao ya Jamii kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Simba kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Mkapa kwa mabao ya Fiston Mayele ambaye amemtungua Beno Kakolanya huku lile la Simba likifungwa na Pape Sakho.

Simba walianza kufunga kipindi cha kwanza mapema dk ya 16 na kuwafanya waongeze hali ya kujiamini mpaka dk 45 zilipokamilika.

Mabadiliko ya Bernard Morrison ambaye aliingia kipindi cha pili na Jesus Moloko yaliongeza nguvu upande wa kiungo.

Zoran Maki alizidiwa mbinu na uzoefu na Nasreddine Nabi ambaye ameweza kuwaongoza vijana wake kupindua meza kibabe.

Previous articleYANGA 0-1 SIMBA,UWANJA WA MKAPA
Next articleAZAMKA INAWALETA ZESCO KESHO AGOSTI 14