NYOTA WAWILI WA ARSENAL KUIKOSA ASTON VILLA

KLABU ya Arsenal inayonolewa na Kocha Mkuu, Mikel Arteta itakuwa kwenye msako wa pointi tatu muhimu ndani ya Ligi Kuu England bila uwepo wa nyota wake wawili.

Ni kipa Aaron Ramsdale pamoja na mshambuliaji Gabriel Martinelli ambao hawakuwepo katika safari ya kuibukia Midlands.

Ramsdale yeye ana maumivu huku Marttinelli anapambania afya yake kwa kuwa anaumwa.

Ina maana kwamba ni Bernd Leno atakuwa chaguo la kwanza huku Emile Smith Rowe atacheza katika nafasi ya ushambuliaji.

Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Villa Park leo Machi 19,2022.