REKODI MWANZO MWISHO LIGI KUU BARA

RAUNDI ya sita ilikuwa ni moto kila kona ambapo ulipigwa mpira mkubwa huku kila timu zikipambana kusepa na pointi tatu.

Kwenye mechi nane jumla ya magoli yamefungwa 22 na mechi mbili zimetoa mabao mengi ilikuwa ni Ruvu Shooting 1-3 Simba na Mbeya City 3-1-dhidi ya Mtibwa Sugar jumla yamepatikana mabao manne

Mechi ya mashuti mengi ni Mbeya City mashuti 12 v Mtibwa Sugar 6 jumla mashuti 18.

Jumla mashuti nje ya lango ni 105  pia timu nyingine ambayo imepiga mashuti mengi nje ya 18 ni KMC dhidi ya Azam FC ilipiga mashuti 13 .

Krosi zilipigwa mara 147 na ile ya Tanzania Prisons v Mbeya Kwanza ilikusanya krosi 25, 10 Mbeya Kwanza

Faulo 258 katika raundi ya 6 na mechi iliyotoa faulo nyingi ni Prisons v Mbeya Kwanza walifanyiwa faulo mara 18 na Prisons 19.

Kadi za njano 28 na mchezo wa Namungo v Yanga ulikusanya kadi 9 za njano pia Prisons,Kagera Sugar timu hizi hazikupewa kadi za njano kwa wachezaji wao.