SIMBA:TUTASHINDA MBELE YA RS BERKANE,WATANZANIA MTUOMBEE

BARBARA Gonzalez, Mtendaji Mkuu wa Simba amesema kuwa wapo tayari wa ajili ya mchezo wao dhidi ya RS Berkane ya Morocco unaoatarajiwa kuchezwa Jumapili na wanaamini kwamba watashinda. Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Pablo Franco, Februari 27 inakibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya RS Berkane kwenye mchezo wa hatua ya makundi wakiwa katika kundi…

Read More

AIR MANULA NI NAMBA MOJA

AISHI Manula, ‘Air Manula’ kipa wa Simba ni namba moja kwa makipa waliokaa langoni kwenye mechi zote 15 za mzunguko wa kwanza na kusepa na clean sheet, (cheza bila kufungwa) nyingi. Manula amekaa langoni kwenye mechi zote 15 ambazo Simba imecheza na amefungwa mabao 6 katika mechi hizo ambazo amekaa langoni. Katika mechi hizo ni…

Read More

MAYELE APEWA ZAWADI YA NG’OMBE

MMOJA wa mashabiki wa Yanga, mwenye asili ya Kimasai anayefahamika kwa jina la Mauya mkazi wa Dakawa, amemzawadia ng’ombe mzima mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele. Mayele ni mtupiaji namba moja ndani ya Yanga akiwa na mabao 7 na kinara ni Relliats Lusajo ambaye ametupia kibindoni mabao 10. Ushindi wa mabao 2-0 waliopata jana mbele ya…

Read More

FT:LIGI KUU:MTIBWA SUGAR 0-2 YANGA

UWANJA wa Manungu Complex mchezo umekamilika na ubao umesoma Mtibwa Sugar 0-2 Yanga. Ni dakika ya 45+5 bao hilo lilipachikwa na kuwafanya Mtibwa Sugar wasiwe na chaguo la kufanya. Mtupiaji wa bao la kuongoza ni Said Ntibanzonkiza ambaye ametumia pasi ya Feisal Salum. Hakuna timu iliyoonyeshwa kadi ya nyekundu huku timu zote mbili zikicheza kwa…

Read More

YANGA HAINA HOFU NA MANUNGU

HASSAN Bumbuli, Ofisa Habari wa Yanga,amesema kuwa Uwanja wa Manungu ambao unatarajiwa kutumika leo kwamchezo wao wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar kwao sio tatizo. Yanga ambao ni vinara wa ligi wakiwa na pointi 36, wanatarajia kukutana na Mtibwa Sugar iliyokusanya pointi 12 na zote zimecheza mechi 14.   Akizungumza na Championi Jumatano, Bumbuli alisema kila mechi wanazocheza kwao ni muhimu bila kujali wanacheza wapi kwa…

Read More

CHEKI MATOKEO YA MTIBWA V YANGA

LEO Februari 23, Uwanja wa Manungu unatarajiwa kuchezwa mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Mtibwa Sugar v Yanga majira ya saa 10:00. Timu hizo zimekuwa na matokeo ya kushangaza kila zinapokutana uwanjani hivyo leo dakika 90 zitaamua nani atakuwa nani. Haya hapa ni matokeo ya mechi za hivi karibuni walipokutana kwenye ligi:- Yanga imeshinda…

Read More

VIDEO;YANGA WABAINISHA KUHUSU UBINGWA

HAJI Manara, Ofisa Habari wa Yanga amesema kuwa kuelekea kwenye mchezo wao wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar unaotarajiwa kuchezwa kesho Februari 23, Uwanja wa Manungu wapo tayari na benchi la ufundi linahitaji ushindi. Manara ameweka wazi kwamba Mtibwa Sugar ilishawahi kuwa bingwa wa ligi mara mbili mfululizo na uzoefu katika kushiriki mashindano makubwa na…

Read More