Simba vs Mtibwa Sugar ni mchezo wa NBC Premier League unaotarajiwa kuchezwa Jumapili, Januari 18,2026. Uwanja wa Mej.Gen. Isamuhyo.
Hii ni baada ya ligi kusimama kwa muda kutokana na mashindano ya AFCON ambayo yanaendelea nchini Morocco na Tanzania iliishia hatua ya 16 bora.
Fainali inatarajiwa kuchezwa Jumapili, Januari 18,2026 itakuwa ni Senegal vs Morocco ambao ni wenyeji.
Kwa upande wa mchezo wa Simba SC vs Mtibwa Sugara unakuwa mchezo wa kwanza kwenye ligi ndani ya 2026 kwa wababe hawa wawili kukutana uwanjani.
Simba SC kwenye msimamo ni nafasi ya 5 ikiwa na pointi 12 baada ya mechi 5. Inakutana na Mtibwa Sugar nafasi ya 7 pointi 10 baada ya mechi 8. Vinara kwenye msimamo ni JKT Tanzania wakiwa na pointi 17 baada ya kucheza mechi 10.
Viingilio
Mzunguko ni 5,000
VIP ni 10,000