>

JE NI NIGERIA AU IVORY COAST FEBRUARI 11 AFCON?

Je ni Nigeria au Ivory Coast siku ya Jumapili fainali ya AFCON?. Hatimaye sasa mbivu na mbichi kufahamika siku hiyo ambapo timu hizo mbili zitakuwa zikiwania ushindi wa Kombe hilo kubwa Barani AFRIKA.

Jumapili ndipo Fainali ya michuano hii ya AFCON 2023 itatamatika kwa kushuhudia fainali kali kati ya Nigeria dhidi ya Ivory Coast ambao ndio wenyeji wa michuano hii.

Imekuwa ni michuano ya kushangaza sana hasa baada ya wale ambao walitarajiwa kufika mbali wakatolewa kwa kushangazwa akiwemo Egypt ambae ni bingwa mara 7 wa michuano hii, Ghana ambaye alisumbua Kombe la Dunia, Morocco ambao alikuwa ni mshindi wa 4 Kombe la Dunia lilipoita, Senegal ambae alikuwa ni bingwa mtetezi wa Kombe hili la AFCON, Algeria na wengine wengi.

Ikumbukwe kuwa Nigeria ambao kwasasa wapo chini ya kocha mkuu Jose Peseiro ni washindi wa Kombe hili mara tatu ambalo walilichukua mwaka 1980, 1994 na mwaka 2013, huku Ivory Coast chini ya kocha mkuu kwasasa Emerse Fae wao wakichukua kombe hili mara mbili pekee Mwaka 1992, na 2015.

Ndugu mteja ukiendelea kuchanganua nani wa kumpa ushindi kwenye Fainali meridinabet wanakwambai cheza michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile Poker, Roullette, Aviator, Sloti na mingine kibao sasa. Ingia na ucheze.

Na sasa ndugu mteja wa Meridianbet tunaenda kuangalia ni kwa namna gani timu hizi mbili Nigeria au kwa jina jingine THE SUPER EAGLES na Ivory Coast kwa jina lingine THE ELEPHANTS walivyofika kwenye hatua hiyo ya Fainali ya AFCON msimu huu kuanzia hatua ya makundi.

HATUA YA MAKUNDI

Kwanza kabisa timu hizi zilikuwa kwenye kundi 1 kwenye michuano hii ya AFCON ambalo lilikuwa ni Kundi A, ambalo lilikuwa na timu nne ikiwemo Guinea Bissau, Equatorial Guinea, Ivory Coast pamoja na Nigeria wenyewe.

Kwenye kundi hilo Nigeria alishika nafasi ya pili baada ya kupata pointi 7 akishinda mechi 2 na kutoa sare 1, huku The Elephants wao wakishinda mechi 1 na kupoteza mechi mbili na kupita kwenye 16 bora kama “BEST LOOSER”

Lakini walivyokutana wao kwa wao Nigeria alishinda mechi hiyo dakika ya 55 baada ya kupata mkwaju wa penati ambao ulifungwa na captain wao Troost-Ekong na kuiptaia timu yao alama 3.

HATUA YA 16 BORA

Ndani ya 16 bora sasa mambo yalikuwa ni moto zaidi ambapo kila timu ilihitaji kushind ambapo Nigeria yeye alipangwa kukipiga dhidi ya Cameroon ambao nao walikuwa ni moja ya timu walipigiwa upatu wa kushinda taji hili lenye thamani kubwa Afrika.

Lakini The Super Eagles walionyesha ukubwa wao kwa kumchapa Camroon kwa mabao 2-0 dakika 90 za mchezo huku mabao hayo yakifungwa na Ademola Lookman mchezaji ambaye anakipiga kule Atalanta ya Italia.

Wakati kwa upande wa Ivory Coast mwenyeji wa michuano hii hatua hiyo alipangwa na na bingwa mtetezi wa michuano hii Senegal ya Sadio Mane ambapo takribani watu wengie walimpa nafasi kubwa Msegali kuondoka na ushindi. Lakini mechi ikawa tofauti na matarajio ya watu baada ya kuishna 0-0 dakika 90 za mchezo na hatimyae kwenda matuta.

The Elephants hatimaye walitinga hatua ya Robo Fainali baada ya kushinda kwa mikwaju ya penati 5-4 na kushangaza walio wengi na kusema kweli mpira ni dakika 90 na filimbi ya mwisho ndiyo itaamua nani ni nani.

HATUA YA ROBO FAINALI

Kwenye hatua hii mechi zilikuwa kali sana kutokana na timu ambazo zilikuwa zimetinga kwenye hatua hii ya Robo Fainali kwani Nigeria yeye safari hii alikutana na Angola ambaye alimchapa bao 1-0 ndani ya dakika 90 za mchezo.

Ivory Coast yeye alikipiga dhidi ya Mali ambao walionekana kuwa wabishi sana kutokana na kikosi ambacho walikuwa nacho. Lakini vijana wa Fae walikuwa wabishi baada ya kushinda kwenye muda wa ziada kwa 2-1 licha ya kuwa na kadi nyekundu 1.

HATUA YA NUSU FAINALI

Timu zote zimecheza michezo yao ya nusu fainali hapo jana huku Nigeria yeye akishinda kwa mikwaju ya penati 4-2 baada ya kwenda dakika 90 kwa bao 1-1 dhidi ya South Africa pongezi zikienda kwa Golikipa wao Nwabi ambaye aliokoa penati tatu. Huku Ivory Coast wao wameingia Fainali baada ya kuichapa DR Congo kwa bao 1-0 dakika 90 za mchezo bao ambalo lilifungwa na Sebastian Haller.

FAINALI HIYO ITAPIGWA JUMAPILI HII

Baada ya kushuhudia mechi mbalimbali za AFCON 2023 sasa tamati ni siku ya Jumapili hii ya tarehe 11 Februari saa 5:00 usiku katika Dimba la Alassane Outtara ambapo Nigeria atazichapa dhidi ya Ivory Coast huku timu zote zikiwa na hamu ya kuchukua Kombe hili 2023.

Nigeria wachezaji wa kuchungwa ni pamoja na Victor Osimhen, Ademola Lookman, Simon, Iwobi na wengine wengi. Huku kwa upande wa Ivory Coast wachezaji wa kuchungwa ni pamoja na Franck Kessie, Sebastian Haller, Sangare na wengine wengi. Je unadhani nani ataibuka kidedea wa kuchukua Kombe hili la AFCON? Osimhen ataibeba Nigeria mabegani? Mechi hii ina ODDS 2.69 kwa 2.79. Suka mkeka wako sasa na meridianbet.

KWA MSHINDI WA TATU SASA

Na pia mechi hizi za AFCON kutakuwa na nafasi ya kugombani mshindi wa tatu kwa timu ambazo zimetoka kwenye nusu fainali ambapo hapa kuna DR Congo na South Africa.

Timu hizi zitagombea mshindi wa tatu siku ya Jumamosi tarehe 10 Februari hii saa 5:00 usiku huku tayari Meridianbet wakiwa wameshakuwekea ODDS kwenye akaunti yao hivyo ingia na ubeti mechi hii.

Meridianbet wamempa nafasi kubwa ya kushinda mechi hii Congo kwa ODDS ya 2.25 kwa 3.38. Wewe beti yako unaiweka wapi kati ya hizi timu mbili?

Mara ya mwisho kukutana timu hizi ilikuwa ni mwaka 2023 kwenye mechi ya kirafiki ambapo South Africa Bafana Bafana alishinda kwa bao 1-0. Je Jumamosi ni siku ya DR Congo kulipa kisasi?. Beti sasa na meridianbet.