KAZI ni nzito kwa wachezaji wa Simba kusaka ushindi mbele ya Power Dynamos katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Oktoba Mosi.
Ikiwa wachezaji wataingia uwanjani kutafuta mabao ya kideo itawagharimu na safari ya kutinga hatua ya makundi itagotea hapo.
Hasara kubwa kwa Simba kutokana na uwekezaji katika usajili msimu wa 2023/24 hasara kwa Taifa kubaki na Yanga katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Kwenye Kombe la Shirikisho Afrika Singida Fountain Gate wanakibarua cha kusaka ushindi dhidi ya Future huku Yanga wakiwa wameandika rekodi nzuri kimataifa.