DAVID de GEA AONDOKA MAN UNITED

BAADA ya kudumu kwa muda miaka 12 ndani ya Manchester United hatimaye ameondoka ndani ya kikosi hicho.

Ni David De Gea ameweka wazi kuwa wamefanikiwa mambo mengi tangu zama za Sir Alex Ferguson.

Nyota huyo mkataba wake umegota mwisho msimu huu na alipewa muda wa kufikiria kusaini mkataba mpya walipokuwa kwenye mazungumzo.

Anatajwa kuwa kwenye hesabu za kuibukia Saudi Arabia kwa ajili ya kuanza changamoto mpya.

Kitambo ndani ya Manchester United hivyo kwa sasa hatakuwa ndani ya United.

Kipa huyo amesema Manchester United ipo ndani ya mtima wake muda wote.